• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 8:55 AM
Mashahidi 43 kuitwa kwenye kesi ya NYS

Mashahidi 43 kuitwa kwenye kesi ya NYS

Na RICHARD MUNGUTI

MKURUGENZI wa mashtaka ya umma (DPP) Jumatano alisema ataita mashahidi 43 kutoa ushahidi katika kesi inayowakabili washukiwa 47 wa sakata ya shirika la huduma ya vijana kwa taifa NYS.

Washukiwa wamekanusha mashtaka ya wizi wa zaidi ya Sh468milioni , matumizi mabaya ya mamlaka na kutozingatia kwa sheria za ununuzi wa bidhaa zilizowekwa na Serikali.

Kiongozi wa mashtaka alimweleza hakimu mkuu , mahakama ya kesi za ufisadi katika mahakama ya Milimani Nairobi Bw Douglas Ogoti kuwa kila shahidi atachukua muda wa masaa mawili kutoa ushahidi dhidi ya washukiwa hao 47.

“Kila mmoja wa mashahidi hawa 43 atachukua muda wa masaa mawili kutoa ushahidi kisha ahojiwe na mawakili 40 wanaowatetea washtakiwa,” hakimu alifahamishwa.

Walioshtakiwa ni pamoja katibu mkuu Bi Lillian Omollo na aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa NYS Richard Ndubai.

Mawakili walisema watachukua muda sawa na huo kila mmoja kuwahoji mashahidi.

Washtakiwa wote 47 walikanusha mashtaka dhidi yao na kuachiliwa kwa dhamana ya Sh8milioni kila mmoja.

Miongoni mwa wale ambao hawajalipa dhamana ni pampja na Bi Anne Wambere Ngirita Bi Anne Wambere Ngirita , baba yake na dada zake wawili.

Mama yao Bi Lucy Ngirita alifaului kumpata mtu wa kumsimamia dhamana.

Wengine wa familia hiyo ya Ngirita hawajalipa dhamana na wanaendelea kuzuiliwa katika gereza la viwandani na Kamiti.

Familia ya Mzee Ngirita iliyoshtakiwa kwa ufisadi huo wa zaidi ya Sh468milioni ingali katika magereza ya Viwandani na Langata mtawalia.

Walioshtakiwa ni pamoja na Bi Anne Wambere Ngirita aliyshtakiwa kupokea Sh60milioni.

Shtaka lilisema kuwa hakuwa ametoa huduma zozote kwa shirika hilo ndipo alipwe pesa hizo.

Washtakiwa hao wamekaa gerezani kwa zaidi ya mwezi mmoja huku wakijikakamua kulipa dhamana hiyo.

Bi Omollo na Bw Ndubai  aliyekuwa mkurugenzi aliondoka siku chache baada ya Jaji Hedwiq Ong’undi kuwapa dhamana  mnamo Juni 19.

Washukiwa 47 wa sakata hiyo ya NYS walishtakiwa kwa makossa mbali mbali.

Kesi inaendelea.

You can share this post!

Mkuu wa Kerra ashurutishwa kulipa wakulima Sh163 milioni

Muthama na Aladwa waomba kesi zao zitamatishwe

adminleo