• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 10:08 PM
Mbunge ateua baraza la mawaziri kumsaidia kazini

Mbunge ateua baraza la mawaziri kumsaidia kazini

Na MARY WAMBUI

MBUNGE wa Thika Mjini Patrick Wainaina amezindua baraza la mawaziri wanane, ambalo litamsaidia kutimiza ahadi alizotoa kwa wakazi wa eneobunge hilo.

Kulingana naye, kundi hilo litaangazia uimarishaji wa uchumi, miundomsingi, kilimo, elimu/talanta, afya, mazingira na hali ya usalama.

Kundi hilo pia litamsaidia kuimarisha hali ya masomo katika shule zote za umma, kufufua sekta ya Jua Kali, kuimarisha usambazaji wa umeme kwa wakazi kati ya masuala mengine.

Akizungumza na Taifa Leo kwa mara ya kwanza, Bw Munene alisema kwamba mkakati huo unalenga kuhakikisha ametekeleza mipango yake ya maendeleo.

“Kaulimbiu yangu ni: Hapa Kazi Tu. Ningetaka kukumbukwa kwa kutoa uongozi bora ambao utachangia kuimarisha maisha ya wakazi. Lazima tuhakikishe kwamba eneo hilo limerejesha hadhi yake kama kitovu cha biashara,” akasema.

 

You can share this post!

Amri ya kubomoa jengo la gavana yakoroga seneta

MAKALA MAALUM: Wiper yaanza kusaka kura za 2022 mapema

adminleo