• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:55 AM
Mswada wa NYS kuwasilishwa bungeni

Mswada wa NYS kuwasilishwa bungeni

Na BERNARDINE MUTANU

BARAZA la Mawaziri limeidhinisha mkataba kutoka Wizara ya Vijana na Huduma za Umma. Mkataba huo ulibuniwa kwa lengo la kuwasilishwa kwa Mswada wa Shirika la Kitaifa la Vijana (NYS) 2018.

Mswada huo una mikakati kadhaa inayolenga kuimarisha operesheni na usimamizi wa NYS miongoni mwa kuleta mabadiliko katika idara hiyo kuifanya shirika la kiserikali.

Zaidi, mswada huo unalenga kuambatisha malengo ya NYS na ajenda nne za maendeleo serikalini (Big 4 Agenda) pamoja na Ruwaza ya 2030.

“Unalenga kukabiliana na udhaifu uliobainishwa katika muundo wa NYS ambao umefanya vigumu utekelezaji mkamilifu wa wajibu wake,” ilisema taarifa kutoka kitengo cha uchapishaji cha rais (PSCU).

Pia, mswada huo unalenga kuziba nyufa katika usimamizi na kufuatilia utekelezaji wa majukumu ya NYS kwa lengo la kudhibiti ufisadi na uhalifu ndani ya shirika hilo.

Katika mkutano ulioendeshwa na Rais Uhuru Kenyatta Ikulu, Nairobi, na uliohudhuriwa na Naibu wa Rais William Ruto Baraza la Mawaziri pia liliidhinisha mwongozo wa utekelezaji wa mradi wa nyumba za bei ya chini, moja ya ajenda nne za maendeleo za serikali ya Jubilee.

You can share this post!

Simu mpya ya Huawei Y9 2019 yatua sokoni

K.U yapoteza mamilioni baada ya TZ na Rwanda kufunga mabewa...

adminleo