• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 12:56 PM
Mwanahabari apatikana amefariki chumbani mwa inspekta mwanamke

Mwanahabari apatikana amefariki chumbani mwa inspekta mwanamke

Na DICKENS WASONGA

MWANAHABARI Eric Oloo ambaye hufuatilia matukio Siaya akiwajibikia gazeti moja nchini amepatikana Alhamisi asubuhi akiwa amefariki katika nyumba ya inpekta mkuu wa polisi mwanamke Ugunja huku afisa huyo akiwa mafichoni.

Maiti ya mwanamume huyo aliyekuwa na umri wa miaka 40 ilikutwa kitandani kukiwa na damu kote.

Afisa huyo, imekuwa imefahamika kwamba alikuwa akiishi naye.

Maafisa wa polisi wamepeleka maiti katika mochwari ya Ambira, amethibitisha kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Ugunja Bw Ibrahim Muchuma bila kutoa maelezo zaidi.

Mfanyakazi wa afisa huyo wa kike amerekodi taarifa kituo cha polisi cha Ugunja.

Afisa mmoja ambaye hafai kuzungumza na vyombo vya habari amesema wanaume wengine walikuwa katika chumba hicho ambapo imetokea farakano Jumatano usiku. Mmoja amekamatwa.

Kamanda wa polisi wa Siaya Bw Francis Kooli amesema mwanahabari alikuwa katika uhusiano wa kimapenzi na afisa.

“Hili ni suala zito hapa Siaya,” akasema.

You can share this post!

Shule zaendelea kufurahia matokeo bora ya KCPE 2019

KCPE: Walimu walia kutumika kama watumwa

adminleo