• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 6:07 PM
Ngome ya Rais Kiambu imechoshwa na handisheki – Kuria

Ngome ya Rais Kiambu imechoshwa na handisheki – Kuria

Na PETER MBURU

MBUNGE wa Gatundu Kusini Moses Kuria sasa anadai kuwa wakazi wa Kaunti ya Kiambu ambako ni ngome ya Rais Uhuru Kenyatta hawataki lolote kuhusu ‘handisheki’ ya Rais na kiongozi wa chama cha ODM Raila Odinga

Mbunge huyo alisema kuwa wakazi hao wanaipinga vikali na kufanya yote wawezayo kuimaliza, maneno ya kushangaza ikizingatiwa kuwa ngome ya Rais ndiyo inatarajiwa kuwa ya kwanza kumuunga mkono.

Katika ujumbe kwenye akaunti yake ya Facebook Jumatatu, Bw Kuria alisema kuwa alizomewa na wakazi hao baada ya kuwasilisha mapendekezo yake kwa timu ya BBI ambayo imekuwa ikizunguka nchini kupokea maoni ya Wakenya.

Alisema japo amekuwa akiunga mkono handisheki, wakazi wa Kiambu na eneo lake, nyumbani kwa Rais hawaitaki.

“Ijumaa niliwasilisha maoni yangu kwa timu ya BBI Kiambu. Jumapili ilikuwa siku mbaya kwangu katika hafla uwanja wa Ruiru wakati watu wa eneo langu walinituma na ujumbe wazi. Hawataki lolote kuhusu handisheki,” akasema Bw Kuria.

Akijitetea kuwa yeye ni shabiki wa muafaka huo wa Rais na Bw Odinga, aliendelea kusema kuwa kwa wakazi wa Kiambu haijawafurahisha.

“Wanaipinga kabisa na wanaikashifu,” akasema, japo katika ujumbe wake akijaribu kuwarai wakazi kutokata tamaa mapema.

Hata hivyo, mbunge huyo alisema ni jukumu la viongozi kuwaeleza watu kuhusu maana halisi ya handisheki, jambo ambalo amekuwa akilalamika kutoka mbeleni kuwa hata viongozi hawaielewi.

“Tusikate tamaa wakati huu. Tufanye juhudi kuwaeleza kuwa handisheki ni kitu kitakachotufaa siku za usoni,” akasema.

You can share this post!

KUPPET yamtetea mwalimu aliyedaiwa kutunga mimba mwanafunzi

AFCON: Kenya na TZ zapokea kichapo sawa

adminleo