• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 7:50 AM
SENSA: Familia kubwa Mandera, Wajir, Marsabit na Garissa

SENSA: Familia kubwa Mandera, Wajir, Marsabit na Garissa

Na VALENTINE OBARA

KAUNTI zilizo Kaskazini Mashariki ya nchi zinaongoza kwa idadi ya watu wanaoishi katika nyumba moja.

Ripoti ya sensa iliyotolewa Jumatatu ilionyesha katika Kaunti ya Mandera, takriban watu saba huishi katika nyumba moja.

Hii ilifuatwa na Wajir, Garissa, Turkana na Marsabit ambazo huwa na takriban watu sita kwa kila nyumba.

Maeneo ya Kati na Mashariki yanayojumuisha Kaunti za Meru, Tharaka-Nithi, Embu, Kitui, Machakos, Makueni, Nyandarua, Nyeri, Murang’a na Kirinyaga familia nyingi zina kati ya watatu na wanne kwa kila nyumba.

Kila nyumba Pokot Magharibi, Samburu, Trans Nzoia, Uasin Gishu, Elgeyo Marakwet, Nandi, Baringo, Laikipia, Nakuru, Narok, Kajiado, Kericho na Bomet zilizo Rift Valley huwa na watu kati ya wanne na watano.

Kwa wastani kitaifa, kila nyumba huwa na watu wapatao wanne isipokuwa Kaunti ya Nairobi ambapo imebainika kwamba nyumba nyingi hazina watu zaidi ya watatu.

Katika eneo la Magharibi, kaunti za Kakamega, Vihiga, Homa Bay, Kisii na Nyamira zina watu wasiopungua wanne kwa kila nyumba. Bungoma na Busia zina karibu watu watano kwa kila nyumba, huku nyumba za Siaya na Kisumu zikiwa na watu wasiozidi wanne.

You can share this post!

SENSA: Pwani walegea chumbani

SENSA: Idadi kubwa ya Wakenya huishi Rift Valley na Mlima...

adminleo