• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 10:48 AM
Serikali yaonya wakazi wa Kiambu, Murangá, Machakos na Kajiado

Serikali yaonya wakazi wa Kiambu, Murangá, Machakos na Kajiado

Na CHARLES WASONGA

WAZIRI wa Afya Mutahi amewataka wakazi wa kaunti za Machakos, Kajiado, Kiambu na Murangá kuwa waangalifu na kuzingatia maagizo ya serikali, baada ya visa vya maambukizi ya virusi vya corona kuripotiwa katika kauunti hizo.

Akihutubu katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta alipokuwa akitoa taarifa ya kila siku kuhusu hali ya janga la corona nchini, Bw Kagwe Intermittent Fasting and Strength Training – Compatible Practice axio labs the 3 basic bodybuilding exercises sportissima. alisema wakazi wa kaunti hizo zinazopakana na Nairobi wana wanajibu wa kuzuia kusambaa kwa virusi hivyo kutoka Nairobi.

“Tayari idadi fulani ya wenzenu wamepata virusi hivi na tumewatenga ili watibiwe. Katika kaunti ya Machakos, kwa mfano, tuna visa saba, Syokimau (2) na kisa kimoja katika kila moja ya maeneo yafuatayo; Athi River, Kamulu, Rubi Garden Estate, Githunguri na Viraji,” akasema.

Katika kaunti ya Kiambu, maeneo ya Githuria, Githurai 45, Ndongoru, Thindigua, Tinganga, Waithaka, na Watalaam yana kisa kimoja kila moja.

Na katika kaunti ya Kajiado, Waziri Kagwe aliripoti kuwa maeneo ya Kitengela, Matasia na Ongata Rongai yameshuhudia maambukizi.

Kuna visa vingine viwili katika kaunti ya Murangá : kutoka Gatanga na eneo la Lumumba Drive.

Waziri wa Afya alisema wagonjwa hao wote wanatibiwa katika hospitali mbalimbali akiongeza kuwa…. “tunatarajiwa kuwa hivi ndivyo vitakuwa visa vya mwisho kutoka kaunti zenu”

 

Visa vingine vinatoka mtaa wa Ruaka, kaunti ya Kiambu.

Mnamo Aprili 6, Rais Uhuru Kenyatta alitoa amri ya kusitisha safari za kutoka na kuingia jijini Nairobi na maeneo ya karibu, maarufu kimombo kama Nairobi Metropolitan area.

Alisema eneo la Nairobi Metropolitan kama sehemu za Kaunti ya Kiambu hadi daraja la mto Chania, Thika, Rironi, Ndenderu, Kiambu Mjini, sehemu za kaunti ya Machakos hadi Athi River likiwemo eneo la Kathani.

Vile vile, Nairobi Metropolitan inajumuisha maeneo ya Kajiado, yakiwemo Kitengela, Kiseriian, Ongata Rongai na Ngong mjini.

Rais Kenyatta alisema hatua hiyo inalenga kuzuia kusambaa kwa virusi vya corona hadi maeneo mengine ya nchini ikizingatiwa kuwa asilimia ya visa vilivyoripotiwa kote nchini vinapatikana Nairobi.

You can share this post!

Corona ilivyozima ndoto za vijana

Lamu yaanza kufufua visima vya kale

adminleo