• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 6:55 AM
Shule ya walemavu yang’aa tamashani

Shule ya walemavu yang’aa tamashani

Na LAWRENCE ONGARO

SHULE ya msingi ya walemavu ya JOY Town, mjini Thika, iliibuka ya pili katika mashindano ya muziki yaliyoshirikisha shule 16 za msingi kutoka eneo la Kati.

Mkurugenzi wa kampuni ya Nut Company Ltd, Bi Anne Mwaura, alisema walemavu wanastahili kupewa nafasi ya kwanza katika mambo yao ya kila siku.

Aliiomba serikali kujitokeza wazi na kuzingatia maslahi ya walemavu hasa wakati wa kutunga mitihani.

“Walemavu wanastahili kupewa muda zaidi wa kufanya mitihani yao kwani hali yao ya maumbile husababisha changa moto tele,” alisema Bi Mwaura, na kuongeza wengi wao huchukua muda mrefu kuelewa mambo.

Alitoa changa moto kwa walimu kuwa mstari wa mbele kuwapa motisha wanafunzi walemavu ili wapige hatua katika masomo yao.

Mwalimu mkuu wa shule ya Joy Town, Bi Mary Wangui Mukami, aliwahimiza wazazi kuwapeleka wana wao walemavu shuleni badala ya kuwaficha kwenye nyumba.

“Ni jambo la kusikitisha kupata ya kwamba wazazi wengi bado huwafungia wana wao manyumbani huku wakiogopa kuchekelewa na jamii. Hii tabia inastahili kukoma mara moja,” alisema Bi Mukami.

Aliyasema hayo mnamo Jumamosi wakati wa fainali ya mashindano ya miziki ya shule za msingi mkoa wa kati, uliofanyika katika shule ya Joy Town mjini Thika.

Shule hiyo iliibuka ya pili kati ya shile 16 zilizoshiki kwa kutunga wimbo uliotajwa kama ‘Ngarisha’.

You can share this post!

Komeni kutumia bunge kulipiza visasi vya kisiasa, arai...

Mbunge apinga wazo la kuondoa shule za mabweni

adminleo