• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 4:55 PM
Wakazi Kisauni wahimizwa wakate bima ya afya

Wakazi Kisauni wahimizwa wakate bima ya afya

Na WINNIE ATIENO

WAKAZI wa Kisauni wamehimizwa kuchukua Hazina ya Bima ya Kitaifa ya Matibabu (NHIF) iwagharimie matibabu wanapougua.

Mbunge wa Kisauni Ali Mbogo alisema waendeshaji bodaboda na madereva wa matatu ni miongoni mwa watu ambao wako hatarini kutokana na kazi yao.

“Wako katika hatari ya kuhusika kwenye ajali maana mtu anaweza kuwa anatoka tu hivi mara gari limegongwa na ajali imetokea hivyo wanafaa kupelekwa hospitalini. Jiandikisheni kwa NHIF ili mtibiwe mkiwa wa wagonjwa na hata wake na watoto wenu watatibiwa,” alisema Bw Mbogo.

Alisema afisi yake itasaidia wahudumu wa sekta ya matatu na bodaboda ili wapate bima hiyo ya afya.

“Nitawalipia kwa mwaka mzima. NHIF ni muhimu sana. Wale hawana vibali wajihimize wawe na stakabadhi hizo muhimu,” alisisitiza.

Kadhalika alisema atawapeleka vijana 600 kujifunza udereva.

Bw Mbogo aliwataka vijana kujitosa katika biashara badala ya kungojea kuajiriwa.

“Pesa haziji kwa kuajiriwa kwa mwezi; biashara ndiyo inaleta maendeleo. Fanya biashara huku ukiwa umeajiriwa,” alishauri.

You can share this post!

Jinsi wabunge wawili walivyojenga shule kipindi cha janga...

Kibwana anuia kusaka urais kwa tiketi ya KLM