• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 11:33 PM
Waliomkejeli Brenda wakamatwe – Kagwe

Waliomkejeli Brenda wakamatwe – Kagwe

Na CHARLES WASONGA

WAZIRI wa Afya Mutahi Kagwe ameamuru polisii kuwakamata watu wanaeneza jumbe za kuwaharibia jina Brenda Cherotich na Brian Orinda kupitia mitandao ya kijamii baada ya kukiri kupona kutokana na Covid-19.

Akiongea nje ya Jumba la Afya House, Nairobi Alhamisi kwenye kikao na wanahabari, Kagwe alilaani vitendo hivyo akisema vinawadunisha wawili hao.

“Nimekerwa mno na baadhi ya Wakenya ambao ambao wamegeukia mitandao ya kijamii kueneza kejeli punde nilipowajulisha kuhusu vijana wetu wawili wamepona kutokana na ugonjwa huo hatari lakini wengine wamedai ni mzaha,” akasema.

“Serikali inawezaje, kwa ushirikiano na Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO), kuamua kuwatumia Wakenya hao wawili kueneza uwongo. Nawataka maafisa wa usalama wawakamate watumiaji mitandao ya kijamii wanaoeneza jumbe kama hizo,” Bw Kagwe akaongeza huku akionekana mwenye hamaki.

Alisema serikali haitavumilia mienendo ya baadhi ya Wakenya kutaja juhudi zake katika kupambana na janga hilo kama shughuli za uhusiano mwema ama hadaa.

Baadhi ya Wakenya ametilia shaka maelezo ya Brenda kuhusu namna alivyopambukizwa na virusi hivyo hadi wakati alipojiwasilisha kwa Hospitali ya Mbagathi.

Wanasema baadhi ya maelezo aliyotoa kwenye mahojiano katika runinga ya NTV yalikinzana na yale aliyotoa katika studio za runinga ya Citizen.

You can share this post!

Sakaja kuongoza kamati ya seneti kuhusu janga la corona

MWANAMKE MWELEDI: Alijitolea kuwapa maskini mikopo nafuu

adminleo