• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 4:55 PM
Wito raia kuwaripoti wanahabari wafisadi

Wito raia kuwaripoti wanahabari wafisadi

NA CECIL ODONGO

TUME ya kupokea malalamishi ya Baraza Kuu la Vyombo vya Habari nchini imewataka raia kupiga ripoti kwake kuhusu wanahabari wafisadi na visa vya kuharibiwa jina kabla ya kuziwasilisha mahakamani.

Kulingana na Mwenyekiti wa tume hiyo Henry Maina, wamiliki wa vyombo vya habari hupoteza kati ya Sh100 milioni na Sh150 milioni kila mwaka kutokana na kesi mahakamani ilhali kesi zenyewe zinaweza kutatuliwa nje ya mahakama.

“Wanahabari siku za nyuma hawajamakinika jinsi wanavyoripoti visa au kuandika habari kuhusu ufisadi. Wao huwalaumu washukiwa hata kabla ya hawajafunguliwa mashtaka mahakamani. Hii huvutia kesi ambazo wanahabari huishia kupoteza,” akasema Bw Maina.

Akizungumza katika mkutano wa kutoa mafunzo kwa wahariri uliofadhiliwa na Chama cha Wahariri nchini jijini Kisumu, Bw Maina aliwaomba wale wote wanaohisi kudhulumiwa na wanahabari, kutosita kuwasilisha malalamishi yao ili tume ifanye uchunguzi na kuwaangushia wahusika adhabu kali. Na Caroline Mundu

You can share this post!

Jinsi ya kutambua dhehebu lenye imani potovu

‘Tangatanga’ sasa wamtetea Ndindi Nyoro

adminleo