2027: Mkutano wa faragha kati ya Gachagua, Wanjigi wazua gumzo
MKUTANO wa faragha kati ya aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua na Kiongozi wa Safina Jimi Wanjigi nyumbani kwake Wamunyoro kunaonekana kuvuruga hesabu za urais ndani ya muungano wa upinzani.
Kumekuwa na madai kwa tikiti ya urais upinzani ni kati ya Kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka na mwenzake wa Jubilee Dkt Fred Matiangi huku Kiongozi wa Linda Mwananchi Edwin Sifuna akitathminiwa kuwa mgombeaji mwenza wa mmoja kati ya wanasiasa hao.
Hata hivyo, kumekuwa na dhana kwamba iwapo hakutakuwa na kigogo wa siasa kutoka Mlima Kenya katika nafasi za juu huenda wapigakura wakakosa kujitokeza debeni.
Bw Wanjigi ametangaza kuwa anasaka urais na kutokana na mfuko wake mzito baadhi ya vinara na wandani wao wameanza kuingiwa na wasiwasi hasa wale wanaoegemea mrengo wa Bw Musyoka.