Barabara za kuelekea Homa Bay kufungwa kesho kwa Madaraka
BARABARA zote zinazoelekea Ikulu Ndogo ya Homa Bay zitafungwa Jumapili Juni 01, 2025 huku kaunti hiyo ikiandaa sherehe za mwaka huu za Madaraka Dei.
Barabara zitakazofungwa ni pamoja na ile ya kutoka Uwanja wa michezo wa Raila Odinga kupitia Kituo cha Polisi cha Homa Bay na ile inayopita Chuo Kikuu cha Tom Mboya.
Barabara inayopita karibu na nyumba za bei nafuu pia itafungwa.Mkuu wa Mkoa wa Nyanza, Flora Mworoa alisema maafisa wa usalama watatumwa kuhakikisha madereva wanafuata maelekezo.
Alisema madereva wanaotoka Kisumu kuelekea Migori lakini hawana shughuli zozote katika Mji wa Homa Bay hawataruhusiwa kupita barabara ya Olare.
Badala yake, magari hayo yataelekezwa kwenye barabara ya Olare-Imbo kabla kuelekea Rodi Kopany na kuungana na barabara ya Homa Bay-Rongo. Barabara hiyo hiyo pia itatumiwa na watu wanaosafiri kutoka Migori hadi Kisumu.