Habari za Kitaifa

Hatuwezi kusimamisha vikao vya Seneti, mahakama yaambia Gachagua

Na MWANDISHI WETU October 15th, 2024 Kusoma ni dakika: 1

NAIBU Rais Rigathi Gachagua amepata pigo mahakamani, baada ya ombi lake la kusitisha vikao vya Seneti vitakavyojadili hoja ya kumtimua mamlakani kutupiliwa mbali.

Akitoa uamuzi wake Jumanne, Jaji Chacha Mwita alisema korti haiwezi kuizuia kazi ya Bunge akisema lina mamlaka ya kisheria kushughulikia masuala yanayowasilishwa mbele yake ikiwemo suala la kutimuliwa kwa naibu rais.

Jaji Mwita badala yake alitaka masuala yaliyoibuliwa kwenye kesi yachanganywe na yale yaliyofikishwa mbele ya jopo la majaji watatu walioteuliwa na Jaji Mkuu Martha Koome Jumatatu.

Jopo hilo linajumuisha majaji Eric Ogola, Anthony Mrima na Frida Mugambi.

Habari zaidi ni kadiri tunavyozipokea…