Ndege yapasuka gurudumu na kuanguka ndani ya Maasai Mara
NDEGE ilianguka Jumatatu, Juni 1, 2026 katika Mbuga ya wanyama ya Olkiombo, Maasai Mara japo hakuna ripoti kuhusu yeyote aliyeaga katika tukio lenyewe.
Kamanda wa Polisi wa Narok Patrick Laboloa alithibitisha kuanguka kwa ndege hiyo saa sita mchana.
Bw Lobola alikuwa ameahidi kuwa angetoa ripoti ya kina kuhusu ajali hiyo baadaye hapo jana.
“Ndege hiyo ilianguka baada ya kupaa kutoka njia yake, gurudumu lake lilipopasuka,” duru ikaarifu Taifa Leo.
Ndege hiyo ilikuwa imewabeba watalii kutoka Nairobi kuelekea Maasai Mara. Bado haikuwa imejulikana idadi ya abiria waliokuwa ndani.
Polisi na uongozi wa Narok hawakuwa wamejibu jumbe na simu kuhusu kisa hicho huku ikisema walikuwa katika sherehe za Madaraka Dei.