• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 6:50 AM
Kenya yakataa wito wa Trump kutwaa mali ya wakuu Sudan

Kenya yakataa wito wa Trump kutwaa mali ya wakuu Sudan

Na MWANDISHI WETU

Kenya imekataa shinikizo za Amerika za kutwaa mali ya viongozi wa Sudan Kusini ambayo inadaiwa ilipatikana kwa njia ufisadi, ulanguzi wa pesa na vita.

Maafisa wa wizara ya Mashauri ya kigeni ya Kenya walisema kwamba Kenya inafurahia kubadilishana habari za kijasusi na Amerika kuhusu pesa haramu kutoka Sudan Kusini, lakini inafaa kuthibitisha ikiwa ripoti kutoka nchi hiyo yenye uwezo mkubwa ulimwenguni ni za kweli.

Katibu wa wizara hiyo Macharia Kamau alisema Kenya ina uwezo wa kutwaa mali yote haramu lakini itafanya hivyo kwa kuzingatia taratibu za kimataifa kupitia kanuni za Umoja wa Mataifa na taasisi za kifedha ulimwenguni.

Wiki jana, Kenya ilishinikizwa na serikali ya Amerika, inayotaka kuona mwisho wa vita Sudan Kusini, kuchunguza na kutwaa mali ya viongozi wa Sudan Kusini ambayo inadaiwa huwekeza pesa za ufisadi nchini.

Utawala wa Rais Donald Trump umezindua mpango wa kuwekea vikwazo viongozi, familia zao na mitandao ya kibiashara na Kenya na Uganda zinatarajiwa kuhusika.

You can share this post!

Uchawi wa kutengeneza pombe haramu wafichuliwa

Tutapunguza ada ya umeme mradi wa Olkaria ukikamilika...

adminleo