• Nairobi
  • Last Updated April 30th, 2024 6:55 PM
Mfungwa aliyejifanya maiti kutoroka jela achomwa hadi kufa

Mfungwa aliyejifanya maiti kutoroka jela achomwa hadi kufa

MASHIRIKA Na PETER MBURU

Maryland, Marekani

JARIBIO la mfungwa kutoroka gerezani eneo la Maryland, Marekani kwa kujificha katika mfuko wa kusafirisha maiti liligonga mwamba vibaya na kusababisha kifo chake Alhamisi, baada ya wafanyakazi wa mochari kumchoma, wakidhani ni maiti.

Gary Smith, 41, alikuwa amekaa ndani kwa miezi 18 ya miaka 12 ambayo alifungwa, baada ya kupatikana na hatia ya kushiriki msururu wa wizi uliofanyika 2014.

Alikuwa amekaa katika gereza la Jessup kwa miezi mitano tu, baada ya kuhamishiwa huko alipojaribu kutoroka kutoka jela ya Brockbridge awali mwaka huu.

Anasemekana kutumia fursa ya mfungwa mwenzake ambaye alikufa, kwa kutupa maiti ya marehemu na kujificha ndani ya mfuko wa maiti, kama mbinu ya kupenya kutoroka nje ya gereza.

Japo mpango wake ulikuwa umefanikiwa, bahati yake haikuwa nzuri kwani kwa kile kinashukiwa kuwa alipatwa na usingizi ama kupoteza fahamu akisafirishwa kupelekwa mochari, alichomwa, wafanyakazi wa mochari wakijua ni maiti.

Lakini akiendelea kuungua wafanyakazi hao walisikia nduru za kutisha, japo walipogundua walimtia mtu hai walikuwa tayari wamechelewa.

“Kulikuwa na mchungu sana katika sauti yake, nduru hiyo ilikuwa ya kutisha. Tulikimbia kuzima kila kitu lakini alikuwa ameungua kabisa hata kabla tufanye kitu,” akasema mkurugenzi wa mochari hiyo Terence Anderson.

Lakini Anderson alisema kuwa mfungwa huyo alikuwa ameachwa peke yake kwa zaidi ya saa tatu katika kitanda cha kusafirisha maiti, akishuku alikuwa amelala ndipo hakutoroka.

Idara za polisi na magereza zimetangaza kufanya uchunguzi wa pamoja kubaini jinsi Smith alitoroka jela na akafa.

Takriban visa saba vya watu walio hai kuchomwa wakidhaniwa kuwa maiti hutokea Marekani kila mwaka.

You can share this post!

Uchu wa kushiriki ngono na mbwa wamuua

Itumbi kulala ndani Muthaiga akisubiri kufikishwa kortini

adminleo