Habari

KQ yarejesha safari za ndege zake kati ya Nairobi na Dubai

Na WINNIE ONYANDO May 14th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

SHIRIKA la Ndege Nchini, Kenya Airways-KQ, imetangaza kuwa ndege zake zitarejelea safari kati ya Nairobi na Dubai katika Umoja wa Milki za Kiarabu (UAE) kuanzia Alhamisi Mei 14, 2026, baada ya kusitisha safari hizo kwa zaidi ya miezi miwili kufuatia kuzorota kwa usalama eneo la Mashariki ya Kati.

Kwenye tangazo mnamo Mei 13, 2026, KQ ilieleza kuwa safari kati ya miji hiyo miwili itakuwa ya kila siku huku likiendelea na mipango ya kuziongeza kutegemea hitaji na wingi wa abiria.

“Tungependa kuwajulisha wateja wetu kuwa safari za ndege kwenda na kutoka Dubai zitarejelewa mnamo Mei 14, 2026. Tutatoa huduma za uchukuzi kila siku kati ya Nairobi na Dubai na tutaongeza safari hizo endapo kutakuwa na hitaji,” shirika hilo likaeleza.

KQ ilikuwa zimesitisha kwa muda safari za ndege hadi Dubai mnamo Februari 28,2026 baada ya nchi kadhaa katika eneo Mashariki ya Kati kufunga anga zao baada ya Amerika na Israel kuanzisha mashambulio dhidi ya Iran.

Iran ilikuwa imejibu kwa kutekeleza mashambulio dhidi ya mataifa kadhaa katika eneo hilo, ambako kuna vituo vya Amerika, kulipiza kisasa.

Miongoni mwa mataifa yaliyolengwa na Iran ni Bahrain, Kuwait, UAE, Qatar na Iran.