Habari

Mishi Mboko aomba Waziri Murkomen akomesha unyanyasaji dhidi ya wanawake

Na ANTHONY KITIMO April 5th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

MBUNGE wa Likoni, Mishi Mboko ameomba Waziri wa Usalama wa ndani Kipchumba Murkomen kuingilia kati na kukomesha ukatili dhidi ya wanawake katika Kaunti ya Mombasa.
Bi Mboko aliambia Bw Murkomen visa vya wanawake kunajisiwa na kuuwawa vimekuwa vikoongezeka katika Kaunti hiyo huku polisi wakionekana kuzembea kupigana na visa hivyo.
Akizungumza walipotembelea Mkurugenzi Mkuu wa bandari William Ruto ambaye amelazwa baada ya ajali ya barabara eneo la Taita-Taveta siku ya Ijumaa mbunge huyo aliomba kusitishwa kwa visa hivyo na washukiwa kukamatwa.
“Tumeshughidia ongezeko wa visa vya ukatili dhidi ya wanawake, kwa muda wa miezi miwili, wanawake watatu wameuwawa bila washukiwa kukamatwa licha ya kupiga ripoti kwa polisi,” alisema mbunge huyo.
Bw Murkomen kwa upande wake alihakikishia mbunge huyo na wanawake wote kuwa vikosi vya Usalama vita wajibika kukomesha visa hivyo.