Habari

Mlimani: Gachagua kumkabidhi Uhuru ripoti hukusu ‘ground’

Na MWANGI MUIRURI July 12th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

MIKUTANO ya siku 45 inaoendelea nyumbani kwa aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua, Wamunyoro, Kaunti ya Nyeri, imeibuka kuwa jukwaa muhimu la kujadili mwelekeo wa kisiasa wa eneo la Mlima Kenya kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2027.
Kwa mujibu wa duru zinazoshiriki katika mashauriano hayo, mojawapo ya mapendekezo yanayojitokeza ni kwamba, Bw Gachagua awanie urais, isipokuwa mahakama iamue kuwa hastahili kushikilia wadhifa wa umma kutokana na kesi yake ya kupinga kuondolewa mamlakani. Mkutano huo ulianza Juni 16 na unatarajiwa kukamilika Julai 31. Katika kipindi hicho, Gachagua amekutana na wajumbe kutoka Mlima Kenya, Nairobi na jamii ya Wamaasai.
Akizungumza Jumamosi alipokutana na viongozi wa Ol Jororok, Gachagua alisema atatayarisha ripoti ya mashauriano hayo na baadaye kukutana na Rais (mstaafu) Uhuru Kenyatta.
 “Baada ya mkutano huu kukamilika nitampelekea Uhuru Kenyatta ripoti ya maoni ya wananchi. Hatutaki kurudia makosa ya 2022 ambapo tuliongoza jamii yetu kwa misimamo tofauti,” alisema.
Alieleza kuwa lengo la mkutano huo ni kusikiliza matarajio ya jamii na washirika wake kuhusu uongozi wanaotaka mwaka 2027 pamoja na masuala wanayotaka yawekwe mbele katika serikali ijayo.