Wantam! Mitandao ya siri ya Gen Z ya kuelekeza siasa za Kenya
KIFO cha Cecil Ouma baada ya hafla ya katibu wa vijana Jacob Fikirini kilifungua ukurasa ambao wengi wa Wakenya hawaufahamu kuhusu siasa za nchi.
Kijana huyo alifariki baada ya kupigwa risasi akiwa ndani ya gari la afisa mkuu serikalini, lakini simulizi ya maisha yake imeibua mjadala kuhusu mtandao wa vijana wanaotumiwa kuhamasisha mikutano ya kisiasa, kulinda viongozi na wakati mwingine kuhusishwa na vurugu.
Kwa wengi, vijana hao hujulikana kama “magenge” au “wahuni”.
Lakini ndani ya siasa, wao hujiita wahamasishaji – watu wanaoweza kukusanya mamia ya vijana kwa muda mfupi kwa mkutano, kampeni au shughuli nyingine za kisiasa.
Hata hivyo, si wahamasishaji wote hufanya kazi kwa maslahi ya wanasiasa.
Wapo pia wanaharakati wa kijamii wanaotumia mbinu hizo kuhamasisha wananchi kuhusu uwajibikaji, haki za kijamii na ushiriki katika uchaguzi.
Mpiga picha Alans Ademba asema kazi yake inaongozwa na lengo, si fedha.