Habari

Pigo kwa wasambazaji wa bidhaa za tumbaku

Na MWANDISHI WETU May 31st, 2025 Kusoma ni dakika: 1

WANAOAGIZA na kusambaza bidhaa za tumbaku nchini wamepata pigo kubwa baada ya Waziri wa Afya Aden Duale kufuta leseni zao.

Waziri huyo pia ameziagiza kampuni zilizoidhinishwa hapo awali kutuma maombi tena ndani ya siku 21.

Bw Duale aliema hayo huku dunia ikiadhimisha siku ya tumbaku.

Sherehe hii ya kila mwaka inafahamisha umma kuhusu hatari za kutumia tumbaku, mazoea ya biashara ya makampuni ya tumbaku, kile ambacho Shirika la Afya Duniani, WHO inafanya ili kupambana na athari za matumizi ya tumbaku.

Nchi Wanachama wa Shirika la Afya Ulimwenguni ziliunda Siku hiyo mnamo 1987 ili kuvutia umakini wa ulimwengu kwa janga la tumbaku na vifo vinavyoweza kuzuilika na magonjwa yanayosababishwa na matumizi ya bidhaa hiyo.

Mnamo 1987, Baraza la Afya Ulimwenguni lilipitisha Azimio WHA40.38, likitaka sherehe hizo zisherehekewe Aprili 7, 1988.

Hata hivyo, mnamo mwaka wa 1988, Azimio WHA42.19 lilipitishwa, na sherehe hizo zikawekwa Mei 31 kila mwaka.