Habari

Ruto: Nitabadilisha sura ya Nairobi kabla ya AFCON 2027

Na KEVIN CHERUIYOT June 30th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

RAIS William Ruto ametangaza kuwa serikali yake inaendelea na shughuli za kubadilisha miundomsingi ya jiji kuu la Nairobi ili kuandaa Kombe la Afrika (AFCON) 2027.

Akizungumza jijini Nairobi jana baada ya kuzindua rasmi mradi wa ujenzi wa barabara inayopita juu ya ile ya Ngong-Naivasha, Rais alisema miradi mingine zaidi iko jikoni.

Alihakikishia Wakenya kuwa nchi iko tayari kuwa mwenyeji wa kindumbwendumbwe hicho cha soka kitakachoanza Juni 19 hadi Julai 17, 2027.

Alisema barabara hiyo yenye urefu wa mita 255 itapunguza msongamano wa magari katika Barabara za Ngong na Naivasha, na kupunguza muda ambao madereva hutumia kwenye msongamano.