Habari

Tutam! Vuguvugu la kumvumisha Ruto 2027 labuniwa

Na PIUS MAUNDU June 29th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

BAADHI ya maafisa wa ngazi ya juu serikalini wameunda vuguvugu la kuvumisha kuchaguliwa kwa Rais William Ruto tena katika uchaguzi mkuu wa 2027.

Kundi hilo linafahamika kama Jamii Imara Mashinani linawajumuisha mawaziri, makatibu wa wizara, wakuu wa mashirika na wakurugenzi wa taasisi za serikali ikiwemo watumishi wengine wa umma.

Wanachama wa kundi hili wamekuwa wakizunguka kote nchini wakivumisha rekodi ya maendeleo ya rais huku kampeni zikishika kasi kuelekea 2027.

“Vuguvugu la jukwaa imara linatoa nafasi na ni jukwaa bora kuwasikiza raia na kuwaeleza kile ambacho nchi imefanya,” akasema Katibu wa Idara ya Ufugaji Jonathan Mueke.

Alikuwa akiongea katika kituo cha kibiashara ya Thokoa, Kaunti ya Kitui, alipowaongoza wajumbe wa serikali kushiriki kikao cha umma na wakazi.

Maafisa hao wa serikali walikumbana na kilio cha raia kuhusu huduma mbalimbali hasa kutoridhishwa kwao na jinsi Mamlaka ya Afya ya Kijamii (SHA) inavyofanya kazi.