Habari Mseto

Kaunti yasifu Sacco kwa kuinua wakazi kiuchumi na kijamii

Na MAUREEN ONGALA September 22nd, 2024 1 min read

SERIKALI ya Kaunti ya Kilifi imesifu mchango wa vyama vya ushirika kwa maendeleo ya kijamii na uchumi.

Naibu Gavana, Flora Chibule alihimiza jamii kujiunga na Vyama vya Ushirika vya Akiba na Mikopo (Sacco) au kuunda vipya kwa sababu manufaa yake yanaonekana.

Akizungumza katika maadhimisho ya miaka 50 ya Imarika DT Sacco mjini Kilifi, alisema Serikali ya Kaunti imebuni mswada ambao utatoa mazingira mazuri ya biashara kwa Sacco.