Bambika

Otile afunguka kuwa hali si shwari, awazia kuacha muziki

Na SINDA MATIKO September 15th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

MWANAMUZIKI Otile Brown amefunguka sababu za yeye kuwa kimya kimuziki kwa muda sasa, akisema kuwa amekuwa akipitia changamoto za kimaisha ambazo zilimpelekea awaze kuachana na muziki.

Otile anasema, katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita, amekuwa akipitia kipindi kigumu sana kimaisha.

“Imekuwa ni kipindi kigumu sana. Nimekuwa nikipambana na mambo mengi sana ya kimaisha na kusema kweli kuna muda niliwaza kuacha muziki kabisa.” anasema Otile.

Ingawaje hakudokeza sababu kwa undani, Otile alidokeza changamoto ya kimuziki akisema sababu kubwa iliyompelekea kuwaza kuachana na muziki ni pesa.

“Sababu kubwa iliyonifanya nisiache muziki ni kwa sababu napenda kutengeneza muziki. Kama ingekuwa nafanya muziki sababu ya pesa ningelikuwa nimeshaacha zamani maana muziki Kenya haulipi. Hamnilipi pesa za kutosha,” akasema.