Kenya ni mchokozi au ni mpatanisha katika ukanda huu?
Mataifa hayo ni kama vile Sudan na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) ambazo zimezongwa na mapigano kwa kipindi kirefu.
Lakini katika miaka ya nyumba, Kenya imefaulu kuongoza michakato ya kuleta amani katika nchi kama Sudan Kusini na Somalia.
Kwa mfano, mapema miaka ya 2000s juhudi za Kenya, kupitia Balozi Maalum Jenerali Elijah Sumbeiyo, zilimwezesha aliyekuwa kiongozi wa waasi John Garanga kuwa rais eneo la Sudan Kusini, na makamu wa rais wa Sudan.
Hii ni baada ya kutiwa saini kwa Mkataba wa Amani mnamo Januari 9, 2025. Hatimaye Sudan Kusini ilitangazwa kama taifa huru, kutoka Sudan, na ikaunda serikali ya mnamo Julai 9, 2011, chini ya Rais wa sasa Salva Kiir.
Kenya pia imechangia pakubwa katika michakato ya kuundwa kwa utawala wa kidemokrasia nchini Somalia.
Kiongozi wa Wiper Kalonzo, wakati huo akiwahudumu katima Waziri wa Masuala ya Kigeni katika serikali ya Rais Daniel Moi, aliongoza mikutano kadhaa mjini Naivasha kujadili amani Somalia.
Juhudi hizi na zingine za kuleta amani katika mataifa mbalimbali zilipandisha hadhi ya Kenya, sio tu barani Afrika bali ulimwenguni, kama mpatanishi mkuu.
Lakini tangu Serikali ya Kenya Kwanza, ilipoingia mamlakani hadhi hii inaonekana kupotea huku Kenya ikichukuliwa kama mchochezi wa uhasama katika mataifa ya ukanda huu.
Hii ndio maana mnamo Juni 27, 2023 miezi michache baada ya Rais Ruto kuingia mamlakani na kuteuliwa na shirika la IGAD kuongoza mchakato wa kuleta amani Sudan.
Lakini kiongozi wa uongozi wa kijeshi wa taifa hilo Jenerali Abdel Fattah Al Burham walimkataa Dkt Ruto akidai anapendelea mahasidi wao- kundi la wapiganaji la Rapid Support Forces (RSF).
Hii ni kutokana na sababu kwamba mapema mwezi huo (Juni 3), Rais Ruto alimpokea balozi maalum wa kiongozi wa kundi hilo Mohamed Hamdan Dagalo katika Ikulu ya Nairobi.
Kwa kukubali kumpokea Yosefu Izzat, ilifasiriwa kuwa Rais Ruto anaunga mkono RSF na juhudi zake za kutaka kuunda serikali sambamba nchini Sudan.
Utawala wa Sudan ulikerwa zaidi na serikali ya Kenya mwaka huu, ilipowaruhusu wafuasi wa RSF kufanya mkutano wao jijini Nairobi.
Mkutano huo ulifanyika Februari 19, mwaka huu katika ukumbi wa KICC, Nairobi, na kuongozwa Jenerali Dagalo, almaarufu Hemedti.
Iliripotiwa kuwa RSF ilitangaza nia ya kuunda serikali sambamba nchini Sudan, hatua ambayo ilikera utawala wa Jenerali Abdel Fattah Al-Burham.
Serikali ya Sudan iliandikia Kenya barua kali ikiishutumu kwa kushirikiana na waasi hao wa RSF kuunda serikali sambamba nchini huo, dai ambalo Kenya, kupitia Waziri wa Mashauri ya Kigeni Musalia Mudavadi, ilikana.
Na mapema mwaka huu (Januari 3, 2025) Rais Ruto alimkaribisha Jenerali Hemedti katika Ikulu ya Nairobi, hatua ambayo iliukera utawala wa Sudan,
Kando na Sudan, Kenya imekemewa na serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kwa kuonekana kuunga mkono Rwanda inatuhumiwa kusaidia kundi la waasi la M23.
Mnamo Januari 15, mwaka huu Rais wa DRC) Felix Tshisekedi aliwashangaza wengi kwa kususia mkutano wa dharura ulioitishwa na Rais William Ruto kujadili njia za kukomesha utovu wa usalama nchini mwake.
Mkutano huo wa marais wa mataifa wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) uliofanyika, kwa njia mtandaoni, Jumatano jioni ulijadili mikakati ya kurejesha usalama mji mkuu mashariki wa DRC, Goma, ulikuwa umetekwa na waasi wa M23 tangu Januari 1, mwaka huu.
Dkt Ruto aliitisha, na kuongoza, mkutano huo kwa misingi ya kwamba ndiye mwenyekiti wa sasa wa jumuiya hiyo, wadhifa aliopewa mnamo Desemba 20, 2024.
Lakini Rais Tshisekedi alihiari kuhudhuria mkutano wa Jumuiya ya Maendeleo ya Mataifa ya Afrika Kusini (SADC) uliofanyika nchini Zimbabwe Januari 30, 2025 ujadili suala hilo hilo la utovu wa usalama mashariki mwa DRC.
Kupitia msemaji wake, Tina Salama, Rais Tsishekedi alisema hivi: “Sitohudhuria mkutano huo kwa sababu unakinzani na shughuli zangu zingine zilizoratibiwa.”
Rwanda imetuhumiwa kwa kuunga mkono na kufadhili waasi wa M23, lakini imekana madai hayo.
Vile vile, Ruto amewahi kujitokeza waziwazi akiitetea Rwanda dhidi ya shutuma hizo.