• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 12:09 PM
LISHE: Ni muhimu kuyala matunda au kunywa juisi ya matunda

LISHE: Ni muhimu kuyala matunda au kunywa juisi ya matunda

Na MARGARET MAINA

[email protected]

INAFAHAMIKA na kuaminika kuwa chakula kina virutubisho ambavyo pia husaidia kuimarisha kingamwili.

Chakula ambacho umekila au unachotaka kukila leo ndicho kinachoamua hali yako kiafya kesho.

Unaweza kuishi bila kuugua kama ukila vyakula vyote muhimu vinavyohitajika mwilini.

Hebu tuangalie juisi zilizotengenezwa kwa matunda na mboga na fadia zake mwilini. Ukweli ni kwamba kuna mchanganyiko wa matunda au mboga aina aina ambazo zina kazi muhimu mwilini na hutumika kama tiba au kinga ya magonjwa.

Vipande vya mananasi na karoti. Picha/ Margaret Maina
Ndizi. Picha/ Margaret Maina

Karoti, tangawizi na tufaha

Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya huondoa sumu mwilini na kuimarisha mfumo wa kinga ya mwili.

Tufaha, tango na figili

Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya ni kinga dhidi ya saratani, huondoa lehemu (cholestrol) mwilini, husafisha tumbo na pia huondoa maumivu ya kichwa.

Nyanya, karoti na tufaha

Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hufanya ngozi ya mwili mzima kuwa nyororo na huondoa harufu mbaya mdomoni.

Tufaha na tango la kawaida

Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya huondoa harufu mbaya mdomoni na hupunguza joto la mwili.

Chungwa, tangawizi na tango

Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hung’arisha rangi ya ngozi na kuifanya kuwa laini. Pia hupunguza joto la mwili. Kwa wale wenye matatizo ya kuwa na ngozi kavu, juisi hii itawasaidia sana.

Nanasi, tufaha na tikitimaji

Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hufanya kazi ya kuondoa chumvi nyingi mwilini, husafisha kibofu cha mkojo na figo. Juisi hii ni nzuri kwa wale wenye matatizo ya kibofu na figo au wanaotaka kujikinga na magonjwa hayo.

Tufaha, tango na ‘kiwi’

Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hung’arisha rangi ya ngozi.

Peasi na ndizi

Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hurekebisha kiwango cha sukari katika damu. Inawafaa sana wagonjwa wa kisukari

Karoti, peasi, tufaha na embe

Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya huzuia athari ya sumu mwilini, hupunguza shinikizo la damu na kuondoa mlundikano wa uchafu mwilini.

Papai, nanasi na maziwa

Juisi hii ina kiwango kikubwa cha Vitamin C, E na madini chuma. Huimarisha rangi ya ngozi na mfumo wa usagaji wa chakula tumboni.

Ndizi, nanasi na maziwa

Juisi hii yenye kiasi kikubwa cha vitamini na virutubisho mbalimbali vyenye faida mwilini, huzuia tatizo la ukosefu wa choo.

Ili kupata faida ya juisi ya matunda hayo, usafi wa matunda yenyewe hauna budi kuzingatiwa wakati wa kutayarisha juisi yake. Vilevile hakikisha unatumia matunda yaliyoiva vizuri.

Unaweza kutumia blenda au kutumia njia ya asili ya kutwanga kwa kinu maalumu na kupata juisi hiyo. Kama utaongeza sukari, unashauriwa kuweka kiasi kidogo sana. Ni bora zaidi usipoweka sukari kwa sababu matunda mengi yana sukari ya asili.

You can share this post!

Manchester United wazamisha Crystal Palace kusalia unyo kwa...

Vituo mbalimbali Busia vyakabiliwa na upungufu wa damu...

adminleo