• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 7:55 AM
MAPISHI: Jinsi ya kupika ndizi na samaki wa kukaanga

MAPISHI: Jinsi ya kupika ndizi na samaki wa kukaanga

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 20

Muda wa kupika: Dakika 30

Walaji: 2

Ndizi. Picha/ Margaret Maina

Vinavyohitajika

  • Ndizi 6
  • Mafuta ya kupikia
  • Samaki 2
  • Kitunguu saumu
  • Chumvi kijiko 1
  • Limau au ndimu 1
  • Pilipili manga
  • Tangawizi 1
  • Vitunguu maji 2
  • Nyanya 2

Maelekezo

Menya na kisha kata ndizi mzuzu vipande vidogovidogo.

Weka kikaangio mekoni, mimina mafuta kwenye kikaangio chenyewe na usubiri yapate moto.

Weka ndizi zikiwa kwenye chombo mekoni, kisha acha kwa muda ziive. Hakikisha unazigeuza ili ziive vizuri pande zote. Weka ndizi zinazotosha ili ziive vizuri.

Ndizi zikiiva, epua na weka kwenye chombo safi kando. Rudia kwa vipande vilivyobaki hadi umalize.

Andaa samaki. Nyunyizia juisi ya limau vizuri juu ya samaki – nje na ndani – kwa uwiano ulio sawa ili samaki apate ladha nzuri. Nyunyiza chumvi vizuri nje na ndani ya samaki.

Ponda kitunguu saumu (au kama una kitunguu saumu cha unga) kisha paka juu ya samaki vizuri, nje na ndani vilevile. Nyunyizia pilipili manga ya unga juu yake na mpake kwa ndani pia. Hakikisha unaweka kiungo hiki tu endapo unakula pilipili kwa sababu kama hutumii pilipili hii hatua si lazima.

Weka tangawizi kwenye samaki. Paka vizuri kwa nje na ndani.

Kata vitunguu maji; weka kwenye kikaangio chenye mafuta ya kupikia. Kaanga hadi viwe vya rangi ya kahawia. Sasa weka nyanya huku ukikoroga.

Zikiiva, weka samaki juu ya vitunguu ili iwe rahisi majimaji yakichuja yanaangukia kwenye vitunguu.

Funika na kwenye moto wa wastani acha chakula chako kipikike kwa dakika 10.

Epua, pakua na ufurahie.

You can share this post!

Sh200m kutolewa kujenga soko la kisasa Githurai 45

SIHA NA LISHE: Cha kufanya ili uwe na ‘umbo...

adminleo