• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 5:01 PM
SIHA NA LISHE: Faida ya kula matango

SIHA NA LISHE: Faida ya kula matango

Na MARGARET MAINA

[email protected]

MWILI wa binadamu unahitaji kuwa na virutubisho vya kutosha.

Virutubisho hivi tunavipata katika vyakula, matunda na hata kupitia katika vinywaji mbalimbali.

Miongoni mwa faida tunazozipata kwa kula matango ni kama zifuatazo:

Kuboresha kiwango cha maji ambayo huhitajika mwilini

Hii ni kutokana na matango kuwa na kiwango kikubwa cha maji. Maji haya husaidia kuondoa sumu mwilini; sumu ambazo tunazipata kupitia vyakula, dawa na hata vinywaji.

Kupunguza uzani wa mwili

Kutokana na matango kuwa na asili ya nyuzi nyuzi, humfanya mlaji ajisikie kushiba bila ya kuongeza vitu mwilini ambavyo husababisha mtu aongezeke uzani.

Hupunguza uchovu

Hii ni kutokana na kuwa na vitamini B na maji mengi; vitu ambavyo vitamfanya mlaji asubuhi asiamke huku akiwa na uchovu.

Husaidia katika mmeng’enyo wa chakula

Matatizo ya tumbo kama vile kuvimba, tumbo kujaa gesi, vidonda vya tumbo na mengineyo hupungua kutokana na ulaji wa matango, husaidia kuondoa sumu tumboni na kurahisisha ufyonzwaji wa protini mwilini .

Husaidia kuondoa msongo wa mawazo

Matango yana kiwango kikubwa cha vitamini B ambayo husaidia kuboresha utendaji kazi wa mishipa mbalimbali ya fahamu mwilini na hivyo kuondoa hatari ya mtu kukumbwa na msongo wa mawazo unaosababishwa na maisha ya kila siku.

Husaidia kuondoa harufu mbaya kinywani

Kwa kukiweka kipande cha tango mdomoni kwa dakika kadhaa, huua bakteria mbalimbali wasababishao magonjwa mbalimbali ya kinywa na harufu mbaya mdomoni.

Tango lina virutubisho vingi na madini muhimu sana katika mwili wa binadamu. tango ni chanzo kizuri cha Kalshiamu, Chuma, Phosphorus Potassium, Zinc, Vitamini B, C na E.

Tango linaaminika kupunguza kiwango cha mafuta mabaya mwilini, huimarisha misuli ya mwili wa ngozi. Watu wengi hutumia tango kwa njia mbalimbali kutunza ngozi zao na kupendezesha sura zao.

Juisi ya tango. Picha/ Margaret Maina

 

You can share this post!

MAPISHI: Jinsi ya kuandaa vipapatio vya kuku vyenye asali

Jinsi serikali inavyolenga kuwaongoza Wakenya kutupilia...

adminleo