• Nairobi
  • Last Updated May 6th, 2024 8:55 PM
SIHA NA LISHE: Ulaji wa tende una manufaa kadhaa katika mwili wa binadamu

SIHA NA LISHE: Ulaji wa tende una manufaa kadhaa katika mwili wa binadamu

Na MARGARET MAINA

[email protected]

TUNDA aina ya tende ni maarufu sana katika mataifa ya Arabuni kama vile Saudi Arabia na Oman.

Ni tunda la mtende ambalo likiwa limeiva huwa na kokwa ngumu yenye rangi baina ya zambarau na kahawia na nyama laini na tamu.

Kwa watu wenye matatizo ya tumbo, tende husaidia kurekebisha matatizo hayo na huleta afueni.

Tende husaidia kuuimarisha mapigo ya moyo

Ondoa mbegu katika tende kisha tumbukiza nyamanyama yenyewe katika maji kwa usiku mmoja na asubuhi kunywa maji hayo. Fanya hivyo mara mbili kwa wiki.

Utafiti umeonyesha kuwa tende husaidia kutanua misuli wakati mwanamke anapokaribia kujifungua, hii husaidia kumfanya mwanamke asipoteze damu nyingi wakati wa kujifungua.

Wataalamu wa vyakula, wanazichukulia tende kama chakula bora kwa wanawake na utafiti wao unaonyesha kwamba husaidia kuyapa maziwa virutubisho muhimu vinavyomfanya mtoto awe na afya njema.

Tende husaidia kupunguza kiwango cha kilevi (alcohol) kwenye damu. Maji ya kunywa ambayo tende imelowekwa ndani yake husaidia kuondoa haraka pombe mwilini.

Tende husaidia kuchelewesha dalili za uzee na pia husaidia kurekebisha ngozi na huondoa mabaka ya kuungua kutokana na athari za jua kali.

Madini ya chuma yanayopatikana katika tende yana umuhimu mkubwa kwa watu wenye upungufu wa damu. Ni ahueni kubwa kwao kula tende.

Vitamin B1 na B2 katika tende husaidia kuyapa nguvu maini.

Tende pia huleta ahueni kwa watu wenye kikohozi na mafua ya mara kwa mara.

You can share this post!

Muthama amkashifu Raila kuhusu kura ya maamuzi

Wanajeshi wawili na polisi wauguza majeraha baada ya...

adminleo