• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 10:15 AM
AFYA: Umuhimu wa ulaji wa maharagwe

AFYA: Umuhimu wa ulaji wa maharagwe

Na MARGARET MAINA na MAJARIDA YA AFYA

[email protected]

MAHARAGWE kwa kawaida ni mbegu za jamii ya kunde lakini kubwa na hupikwa kama chakula au kitoweo. Ni chakula ambacho baadhi ya watu hukichukulia kama chakula cha hadhi ya chini kisichokuwa na manufaa kiafya.

Hata hivyo, maharagwe yana faida nyingi sana mwilini ambazo watu wasiokula maharage kama yanavyojulikana pia, huzikosa.

Maharagwe hupunguza lehemu (cholesterol)

Moja kati ya vyakula vinavyopunguza lehemu mwilini ni maharagwe. Nyuzinyuzi zinazopatikana kwenye maharagwe hujishikiza na lehemu ziwapo tumboni na kuzuia lehemu zaidi kufyonzwa na kuingia mwilini ovyo.

Huboresha afya ya ubongo

Thiamine pamoja na Vitamini K zinazopatikana kwenye maharagwe husaidia katika kuboresha afya ya ubongo.

Husaidia katika kudhibiti kiwango cha sukari mwilini

Kwa kiasi fulani, maharagwe yana nyuzinyuzi ambazo hupunguza kiwango cha metaboli ya wanga (carbohydrates) mwilini. Kwa kufanya hivi, huwezesha kutawala kuongezeka kwa kiwango cha sukari hasa baada ya kula chakula.

Maharagwe pia yana protini ambayo husaidia kupunguza kiwango cha sukari mwilini.

Huongeza nguvu za mwili

Kuwepo kwa madini ya chuma pamoja na manganese kwenye maharagwe kunayafanya kuwa na nafasi kubwa katika kuongeza nguvu za mwili.

Madini haya ni muhimu sana katika kuuongezea na kuupa mwili nguvu.

Huimarisha mifupa

Madini ya calcium pamoja na manganese ni muhimu sana kwa ajili ya afya ya mifupa. Maharagwe ni chanzo kizuri cha madini haya.

Huboresha ngozi

Maharagwe husaidia michakato ya metaboli ya asidi ya amino, gluconeogenesis, neurotransmitter synthesis, histamine synthesis, asidi ya mafuta (fatty acids), lipids and hemoglobin synthesis kwenda vizuri.

Huboresha afya ya macho

Madini ya zinc yanayopatikana kwenye maharagwe ni muhimu sana kwa ajili ya afya ya macho. Hivyo basi ulaji wa maharagwe mara kwa mara utaboresha afya ya macho yako.

Huboresha uwezo wa kumbukumbu

Vitamini B1 inayopatikana kwenye aina mbalimbali za maharagwe hukabili ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu (Alzheimer’s na Dementia).

Huboresha afya ya kucha na nywele

Biotin, madini ya chuma pamoja na protini; vyote vikipatikana kwenye maharagwe, vina nafasi kubwa katika kukupa kucha imara pamoja na nywele zenye afya njema.

You can share this post!

Watano watemwa Migne akitaja kikosi cha Afcon

Wachina wavamia Gikomba, Nyamakima na Kamukunji kuuza...

adminleo