Habari Mseto

Mama wa miaka 22 akana kumuua mwanawe

December 13th, 2018 1 min read

Na RICHARD MUNGUTI

HAKIMU mwandamizi Bi Martha Mutuku Jumanne aliamuru idara ya urekebishaji tabia iwahoji familia ya Bi Mercy Chepng’eno Ruto kubaini hali yake kabla ya kuamuwa ikiwa ataachiliwa kwa dhamana.

Mercy, mwenye umri wa miaka 22 aliyeshtakiwa kwa kuumua mwanawe alisema ,” mimi ni mgonjwa na sikuua.”

Bi Mutuku alitoa agizo hilo baada ya Mercy kuomba aachiliwe kwa dhamana katika kesi ambapo ameshtakiwa kumuua mtoto wake mwenye umri wa miezi minne.

Hakimu mwandamizi Bi Martha Mutuku.Picha/RICHARD MUNGUTI

Mercy alikanusha kuwa alimuua mwanawe Achim Kipkorir mnamo Oktoba 21 2018 katika eneo la Olenguruone.

Mercy alisema hakumuua mwanawe ila “ alifariki kwa sababu ya ugonjwa.”

“ Hii mahakama itaamua ikiwa mshtakiwa ataachiliwa kwa dhamana baada ya ripoti ya afisa wa urekebishaji tabia kuwasilishwa kortini,” alisema Bi Mutuku.

Kesi hiyo iliorodheshwa kutajwa baada ya wiki mbili.