• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Makahaba wakongwe sasa watia chipukizi wa Arsenal mtegoni

Makahaba wakongwe sasa watia chipukizi wa Arsenal mtegoni

Na CHRIS ADUNGO

KIUNGO chipukizi wa Arsenal, Joe Willock, 20, amekiri kukoseshwa usingizi na idadi kubwa ya makahaba ambao kwa sasa wameanza kumtia kishawishini tangu afichue azma ya kumvisha mwanamitindo Eglantine Flore Aguila pete ya uchumba.

Mbali na Eglantine, vipusa wengine wanaowania penzi la Willock ni Dianne Buswell, Pamela Anderson na Kendra Lust aliyewahi pia kutoka kimapenzi na James Rodriguez wa Real Madrid na timu ya taifa ya Colombia.

Eglantine ambaye ni kahaba maarufu mzaliwa wa Ufaransa, amewahi pia kuwafungulia wanasoka Ashley Cole na Mario Balotelli duka lake la asali kabla ya kuanza kutambaliwa na Willock.

Hadi alipomchezesha Willock miereka ya chumbani kwa mara ya kwanza, Eglantine alikuwa akitoka kimapenzi na mwanamasumbwi Amir Khan, fowadi Saido Berahino wa Stoke City na aliyekuwa kiungo wa Manchester United, Marouane Fellaini.

Katika mahojiano yake na gazeti la The Sun wiki jana, Willock alikiri kupagawishwa na weledi wa mchezo wa Eglantine chumbani na kubwa zaidi katika maazimio yake kwa sasa ni kumfanya kichuna huyo mwenye umri wa miaka 27 kuwa wake wa halali.

Willcok amewahi pia kujirinia asali mzingani mwa mwanadensi maarufu mzawa wa Australia, Dianne Buswell aliyetemana na mchumba wake Anthony Quinlan mwishoni mwa mwaka jana.

Awali, Eglantine alikuwa amepasua mbarika kuhusu uhusiano wake na Willock kupitia mtandao wa Instagram kwa kusisitiza kwamba kwa sasa penzi lake limepata hifadhi salama na ya kudumu moyoni mwa tineja huyo matata wa Arsenal japo ‘hakumfanyia kazi nzuri’ walipovaana kwa mara ya kwanza kimahaba.

Katika ujumbe wake, Eglantine alipakia pia picha alizopigwa kwa pamoja na Willock huku mengi ya mabusu aliyokuwa akilirushiwa na ‘dume’ lake yakiashiria ukubwa wa kiwango cha kukomaa kwa penzi lao.

Kipusa huyo aliungama kwamba alimfungulia Willock buyu lake la asali kwa mara ya kwanza kuelekea mwisho wa msimu jana wakati Arsenal walipowazuru Blackpool kwa mechi ya raundi ya tatu ya Kombe la FA uwanjani Bloomfield Road.

Katika mchuano huo, Willock aliwafungia waajiri wake mabao mawili na kuchangia ushindi wa 3-0 uliowapa Arsenal tiketi ya kuvaana na Manchester United waliowadengua baadaye katika raundi ya nne ya Kombe la FA.

Ungamo la Eglantine lilimweka Willock kwenye ‘kurasa mbovu’ za madaftari ya wachanganuzi wa soka ambao kwa sasa wanahisi kwamba huenda chipukizi huyo akapotoshwa zaidi kimaadili na Eglantine asiyetosheka kirahisi na huduma za chumbani.

Mnamo 2015, Eglantine alikiri kutoridhishwa na mchezo wa aliyekuwa beki wa Chelsea na timu ya taifa ya Uingereza, Cole huku akiungama kuwa tunda lake limewahi pia kudokolewa pia na mvamizi wa sasa wa Brescia nchini Italia, Mario Balotelli.

You can share this post!

Sodoma na Gomora mitaani

WANDA AWINO: Niliipenda Sarafina, sasa nalenga kumfikia...

adminleo