• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 4:42 PM
Matokeo mseto kwa klabu za Kenya voliboli Misri

Matokeo mseto kwa klabu za Kenya voliboli Misri

Na GEOFFREY ANENE
KLABU za Kenya zimeanza mashindano ya voliboli ya Klabu Bingwa Afrika ya wanaume na matokeo mseto jijini Cairo, Misri, Jumanne.

Mabingwa wa Kenya,  General Service Unit (GSU) wamekaribishwa mashindanoni kwa kubwagwa na Olympique ya Algeria kwa seti 3-1 za alama 20-25, 25-15, 24-26 na 17-25. Washindi hawa wa medali ya shaba mwaka 2005 watapiga mechi ya pili Machi 28 dhidi ya Wolaitta Dacha ya Ethiopia.

Prisons, ambayo ilinyakua medali ya fedha mwaka 2013, imeanza vyema kwa kunyamazisha Red Skins kutoka Ushelisheli 3-0 (25-15, 25-14, 25-22). Mabingwa hawa wa zamani wa Kenya watapambana na Espoir ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika mechi ya pili Machi 28.

Katika mechi zingine zilizosakatwa Jumanne,  ilikuwa Port (Cameroon) 3 Wolaitta (Ethiopia) 1, DGSP (Congo Brazzaville) 1 Swim Blue (Ushelisheli) 3, Swehly (Libya) 3 Bafia (Cameroon) 0, Ahly Benghazi (Libya) 3 University of Zimbabwe (Zimbabwe) 0, Police (Benin) 3 Mwangaza (DR Congo) 1, Aviation (Misri) 3 Finances (Benin) 0, Smouha (Misri) 3 FAP (Cameroon) 0.

You can share this post!

Okumbi apigwa kalamu kwa matokeo duni ya Harambee Stars

Redio 24 Uganda zafungwa kwa kupeperusha matangazo ya uchawi

adminleo