Habari za Kaunti

Mpox: Kenya yathibitisha kisa cha nne

Na BENSON MATHEKA August 31st, 2024 1 min read

KENYA imethibitisha kisa cha nne cha maambukizi ya ugonjwa wa Mpox huku maafisa wa afya wakihimiza raia kuwa waangalifu.

Katibu wa Afya ya Umma na Viwango vya Kitaalamu Mary Muthoni alisema kisa hicho cha nne kilithibitisha kaunti ya Nakuru baada ya vingine vitatu kuthibitishwa katika kaunti za Taita Taveta, Busia na Nairobi.

Katibu Muthoni alisema kwamba sampuli 90 zilichunguzwa katika Maabara ya Kitaifa ya Afya ya Umma ambapo visa hivyo vinne vilithibitishwa kufikia Jumamosi huku matokeo kuhusu visa vingine viwili yakisubiriwa.

Watu 599,380 walikuwa wamekaguliwa katika vituo 26 vya kuingia nchini kufikia Jumamosi Agosti 31, 2024.