Michezo

Pasta aitisha waumini Sh200,000 aombee Nigeria kufuzu

June 25th, 2018 1 min read

Na AFP

LAGOS, NIGERIA

PASTA ameshangaza wengi kwa kuambia waumini wake wamlipe zaidi ya dola 2,000 (Sh200,000) ili kuombea wachezaji wa timu ya taifa ya kandanda wanaoshiriki katika dimba la kombe la dunia nchini Urusi.

Mhubiri huyo anayejitambulisha kama mtume Tommy Yisa Akia, alisema atatumia pesa hizo kufadhili kikosi cha “mashujaa wa injili” kuombea timu hiyo ya Super Eagles.

Awali alikuwa amedai timu hiyo ilishindwa na Croatia katika mechi yake ya kwanza wiki iliyopita kwa sababu inaadhibiwa na Mungu kwa kuajiri mkufunzi mzungu, Gernot Rohr.

Lakini alisema anaamini Nigeria inaweza kubadili hali yao katika kombe la dunia na kuwa timu ya kwanza Afrika kushinda kombe hilo kama atalipwa pesa hizo.

“Ninahiotaji pesa hizo kidogo ili kununua vifaa kadhaa vya kidini na pia kulipa kikosi changu cha waombaji marupurupu kidogo,” alinukuliwa kusema na mashirika ya habari.

-Imekusanywa na Valentine Obara