Dondoo

Polo ashtuka kipusa wake ‘kunywesha’ majoka maji usiku


KIPKELION, KERICHO

POLO wa hapa alishtuka demu wake alipomwambia kuwa anaweka maji nje ya nyumba usiku ili nyoka hatari wanywe na kuenda zao.

Inasemekana polo alimtembelea kipusa huyo na usiku kabla walale kipusa aliweka maji kwenye mikebe midogo kisha kuiweka kuzingira nyumba yake.

Jombi akamhoji kuhusu hatua hiyo naye akampa jibu lililomtia tumbojoto.

“Hapa kuna nyoka kadhaa na usiku hutambaa wakitafuta maji msimu huu wa kiangazi. Wakipata maji nje wanakunywa na kurudi lakini wakikosa huingia hadi ndani ya nyumba,” kipusa akamjibu.

Polo alikubali jibu hilo lakini baadaye aliambia marafikize kuwa anashuku uhusiano wa demu huyo na wanyama hao.

Balaa shambaboi akitishia kuanika mke wa bosi kwa kumnyemelea

KIVAA, MASINGA

MAMA wa hapa alijuta baada ya shamba boi kutishia kumshtaki kwa mumewe kwa kumnyemelea awe mpango wake wa kando.

Penyenye zinasema kuwa jamaa na mume wa demu huyo ni marafiki wa chanda na pete na jamaa hakutarajia mama huyo angemrushia mistari ya mahaba.

Juzi, demu alishangaza alipomtembelea jamaa kwake na kufungua moyo kumtongoza huku akimuahidi mengi mazuri iwapo atakubali ombi lake.

Hata hivyo, jamaa alipandwa na mori na kumsuta mke wa bosi wake.

“Ninakuheshimu kama mke wa bosi wangu kumbe una mawazo tofauti. Umenifuata hapa kwangu kuniambia hivyo? Tafadhali ione nyumba yangu paa mara moja. Nikome kabisa. Nitakuripoti kwa mumeo,” jamaa alizusha na demu akamlilia asifanye hivyo.