• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Msituhusishe kwa mzozo wenu, Mutula awaambia vinara wa NASA

Msituhusishe kwa mzozo wenu, Mutula awaambia vinara wa NASA

Na PIUS MAUNDU

KIRANJA wa Wachache Seneti Mutula Kilonzo Junior ameonya vinara wa Muungano wa NASA dhidi ya kuwahusisha maseneta na mzozo wao.

Seneta huyo alisema hatima ya Seneta Moses Wetangula tayari imeamuliwa akiongeza kuwa uamuzi wa kumwondoa mwenzao ambaye ni “anajionyesha kuwa bora” hauwezi kubatilishwa.

Baadhi ya wahusika wa Nasa wamewakosoa maseneta wa upinzani kwa kuendesha ‘mgawanyiko’ wa upinzani baada ya kuamua kumng’oa Bw Wetangula kama Kiongozi wa Wachache Seneti.

Nafasi hiyo walimpa Seneta wa Siaya, James Orengo, hatua ambayo pia haijawafurahisha vinara wa muungano.

Kinara wa Nasa Raila Odinga na naibu wake Kalonzo Musyoka wamemsihi Bw Orengo asikubali kuangamiza Nasa kwa kukubali kuchukua nafasi hiyo, maoni ambayo yameibua hisia kali kutoka kwa maseneta ambao ni pamoja na Bw Kilonzo Junior.

“Vinara wa Nasa wanastahili kukoma kuona maseneta wanahusika katika vita vyao,” alisema Seneta huyo wa Makueni.

Bw Kilonzo pia alizungumzia wajibu wake katika utaratibu huo wa kumuondoa Bw Wetangula.

“Wajibu wangu ulikuwa kuwasilisha hoja ya kumuondoa Seneta Wetangula kama inavyoelezwa katika sheria bila hofu ama mapendeleo,” alieleza Taifa Jumapili.

Pia alionekana kupuuzilia mbali juhudi zinazoendelea katika muungano huo wa upinzani kumrejesha Bw Wetangula, na kuonekana kudumisha kuwa uamuzi huo hauwezi kubadilishwa.

 

You can share this post!

Wavuvi wa Kenya wavamiwa tena na polisi wa Uganda

Atakayefichua mwanamume anayewatapeli wabunge kutuzwa...

adminleo