• Nairobi
  • Last Updated April 16th, 2024 12:47 PM
Mtihani wa  handisheki Jubilee ikiingia Kibra

Mtihani wa handisheki Jubilee ikiingia Kibra

Na CECIL ODONGO

USHIRIKIANO kati ya Rais Uhuru Kenyatta na Kinara wa ODM Raila Odinga unatarajiwa kutiwa kwenye mizani baada ya chama cha Jubilee kutangaza kwamba kitakuwa mwaniaji kwenye uchaguzi mdogo wa Kibra hapo Novemba 7.

Katibu Mkuu wa Jubilee, Raphael Tuju alisema wanachama wa Jubilee ambao wangependa kurithi kiti hicho kilichokuwa kikishikiliwa na marehemu Ken Okoth, watume maombi kwa bodi ya uchaguzi ya chama hicho.

“Kufuatia mashauriano na uongozi wa Jubilee kuhusiana na uchaguzi mdogo wa eneobunge la Kibra Novemba 7, tungependa kuwaeleza wanachama wetu kwamba tutawasilisha mwaniaji wetu. Utathmini wetu umeonyesha kuwa chama kipo imara na kinaweza kutoa ushindani mkali kwa wawaniaji wengine,” ikasema taarifa ya Bw Tuju.

Bw Tuju alisema uamuzi huo umepigwa jeki na ushindi wa Nixon Korir katika eneobunge jirani la Langata kwenye uchaguzi wa 2017, kinyume na dhana kwamba eneo hilo lilikuwa ngome ya ODM.

Hata hivyo, taarifa hiyo haikubainisha masharti ambayo wenye azma ya kugombea kwa tiketi ya Jubilee wamewekewa kili kupewa tiket hiyo.

Huku hayo yakiendelea, chama cha ODM nacho kinatarajiwa kupokea vyeti vya wawaniaji leo kisha kuwaidhinisha watakaoshindana kwenye mchujo utakoafanyika Jumamosi hii.

Mwenyekiti wa Bodi ya Uchaguzi wa ODM, Judy Pareno., ambaye pia ni Seneta wa k,uteuliwa, anatarajiwa kuongoza maafisa wenzake kupokea vyeti hivyo, siku mbili tu baada ya Bw Odinga kuongoza hafla ya kuwatambulisha wawaniaji hao 24 kwa wananchi katika uwanja wa Kamkunji, Kibra.

You can share this post!

Sensa ya visanga

SHAIRI: Tumpe jina gani?

adminleo