Habari Mseto

Tanzia tisa wakifariki ajalini Kisumu

Na VITALIS KIMUTAI September 3rd, 2024 1 min read

ABIRIA tisa walifariki dunia papo hapo katika ajali ya barabarani iliyotokea kwenye barabara kuu ya Kericho-Kisumu Jumanne, Septemba 3, 2024.
Ajali hiyo ilihusisha trela na matatu zilizokuwa zinasafiri kwenye barabara ya Muhoroni-Kipsitet katika mpaka kati ya Kaunti ya Kisumu na Kericho.
Taarifa ya polisi ilisema kuwa dereva wa trela alipoteza mwelekeo wa gari lake lililogonga matatu iliyokuwa ikielekea upande tofauti.
“Kutokana na mgongano huo, abiria tisa – wanawake wanne na wanaume watano walikufa papo hapo,” walisema polisi kupitia taarifa.
Idadi isiyojulikana ya manusura walisemekana kukimbizwa katika hospitali ya Muhoroni kwa matibabu. Hali yao haingebainishwa mara moja.
Dereva wa matatu iliyohusika kwenye ajali hiyo karibu na eneo la Ndogo, Kisumu, ni miongoni mwa walioangamia papo hapo huku dereva wa trela akisemekana kutoweka. Hakuwa amepatikana wakati taarifa hii ilipochapishwa.