Habari za Kaunti

Watu watano wafariki, wanane wajeruhiwa ajalini Nakuru

May 25th, 2024 1 min read

NA MERCY KOSKEI

WATU watano walifariki dunia matatu walimosafiria ilipohusika katika ajali eneo la Magaa kwenye barabara ya Eldoret-Nakuru.

Kamanda wa polisi kaunti ya Nakuru Samuel Ndanyi alisema watu wanane walijeruhiwa wakati matatu hiyo iliyokuwa ikielekea Nakuru kutoka Eldoret ilipogongana na lori mwendo wa tisa na nusu usiku wa kuamkia Jumamosi.

Alisema waliofariki katika ajali hiyo ni wanawake wanne na mwanamume mmoja.

“Waliojeruhiwa walipelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Nakuru kutibiwa na mili ya waliofariki dunia imehifadhiwa katika mochari ya hospitali ya kaunti ya Nakuru,” alisema Bw Ndanyi.