• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 7:50 AM
Mbuga ya Maasai Mara bado namba wani Afrika

Mbuga ya Maasai Mara bado namba wani Afrika

Na GEORGE SAYAGIE

MBUGA ya wanyamapori ya Maasai Mara kwa mara nyingine imeorodheshwa katika nafasi ya kwanza Barani Afrika kwenye tuzo za Utalii duniani, World Travel Awards.

Ufanisi huo wa kupigiwa mfano sasa unaiweka pazuri sekta ya utalii nchini haswa baada ya kipindi kigumu cha uchaguzi uliojaa utata mwaka jana na kuathiri sana sekta hiyo.

Kando na Maasai Mara, nyota hiyo ya jaha pia iling’aa katika hoteli za kitalii na hifadhi nyingine za wanyamapori nchini zilizoshinda tuzo za hadhi Kwenye sherehe iliyoandaliwa katika hoteli moja mjini Durban, Afrika Kusuni Jumapili.

Maasai Mara ambayo ni maarufu kote duniani ilichukua nafasi ya sita ulimwenguni na kuzibwaga hifadhi maarufu katika mataifa ya Afrika Kusini, Tanzania na Uganda. Vile vile mbuga hiyo inayopatikana katika Kaunti ya Narok imekuwa ikishinda tuzo hiyo kwa miaka minne mfululizo tangu mwaka 2013.

Kwenye kitengo cha mataifa, Kenya ilishinda tuzo za ufuo bora, mbuga bora ya wanyamapori na tuzo ya bodi bora ya kitalii barani Afrika, ufanisi ambao wamepata miaka ya 2013, 2014, 2015, 2016 na sasa 2017.

Hoteli ya kifahari ya Villa Rosa Kempinsky ilitajwa bora zaidi barani Afrika kwa kutoa huduma zinazoana na tamaduni ya wazungu pamoja na ukarimu wa Wakenya wanaofanyakazi hotelini humo.

You can share this post!

Kura ya maamuzi kupunguzia Wakenya gharama ya maisha...

Gavana Kiraitu akana kuwashauri wakulima wasipande miraa

adminleo