• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 9:40 PM
Wakazi wa Nairobi kutozwa ushuru zaidi

Wakazi wa Nairobi kutozwa ushuru zaidi

Na BERNARDINE MUTANU

WAKAZI wa Kaunti ya Nairobi watalipa ushuru zaidi kutokana na kuanzishwa kwa aina mpya za madaraja ya ushuru na ushuru wa ziada katika baadhi ya sekta kupitia kwa mswada wa fedha ambao umependekezwa.

Hii ni kwa lengo la kujazilia pengo la bajeti ya 2018/2019.

Kutakuwa na ushuru mpya katika uokotaji wa takataka mitaani ambapo wanaoishi katika mitaa ya mabanda watalipa Sh100 kila mwezi.

Watu wanaoishi katika mitaa ya wastani watalipa Sh300 kwa mwezi ilhali wanaoishi katika mitaa ya kifaharu watalipa Sh500 kwa mwezi.

Shule pia zitalipa ada hiyo ambapo shule za kutwa, chekechea na zilizo na wanafunzi zaidi ya 850 zitatakiwa kulipa Sh30,000 kwa mwezi mmoja.

Shule za msingi za mabweni, sekondari, vyuo viku na taasisi za mafunzo ya juu zilizo na wanafunzi zaidi ya 2,000 zitalipa kufikia Sh65,000.

Kuegesha magari ya kibinafsi kutagharimu Sh400 kutoka Sh300 kwa siku.

Huenda mashine zote za ATM jijini zikatozwa ushuru, mabango ya matangazo yataongezewa ushuru pamoja na michezo ya kujipumbaza na bahati nasibu.

You can share this post!

Warsha kuandaliwa kuelimisha timu za KPL msimu mpya ukinukia

Two Rivers yatajwa makao makuu ya Samsung barani Afrika

adminleo