Habari za Kitaifa

Wandani wa Raila wajiunga na serikali

Na BENSON MATHEKA July 24th, 2024 1 min read

WANDANI wa kiongozi wa ODM Raila Odinga wamejiunga na serikali ya Kenya Kwanza.

Rais William Ruto amemteua mwenyekiti wa ODM John Mbadi kuwa Waziri wa Fedha kuchukua nafasi iliyoachwa na Profesa Njuguna Ndung’u, Kiongozi wa Wachache Bungeni Opiyo Wandayi (Kawi), Naibu kiongozi wa ODM Hassan Joho (Madini na Uchumi wa Baharini), Naibu kiongozi wa kwanza wa ODM Wycliffe Oparanya (Ushirika).

Rais Ruto amewateua upya waliokuwa mawaziri Salim Mvurya (Uwekezaji na Biashara), Rebecca Miano (Utalii) Onesmus Murkomen (Michezo ), Alfred Mutua (Leba) huku aliyekuwa Mwanasheria Mkuu Justin Muturi akiteuliwa waziri wa Utumishi wa Umma.

Bi Stella Langat ndiye waziri mteule wa Jinsia.