Habari za Kitaifa

Mwanamke, watoto 4 wafariki ajalini wakielekea Nakuru

Na MERCY KOSKEI August 13th, 2024 1 min read

MWANAMKE na watoto wanne, walifariki Jumanne, Agosti 13, 2024 katika ajali ya barabarani iliyohusisha gari la kibinafsi na lori, iliyotokea eneo la Mbaruk kwenye Barabara Kuu ya Nakuru-Nairobi.

Kamanda wa Polisi wa Kaunti Ndogo ya Gilgil, Bw Jamleck Ngaruiya, alisema gari hilo aina ya Mercedes, lilikuwa likielekea Nakuru lilipogongana na lori.

Kulingana na polisi, gari hilo la Mercedes lilikuwa na watu sita, ambao ni dereva, mwanamke, na watoto wanne.

Kwa bahati mbaya, mwanamke huyo na watoto wanne walikufa papo hapo.

Eneo la ajali Mbaruk, Gilgil katika barabara ya Nakuru-Nairobi ambapo watu watano walipoteza maisha baada ya gari lao aina ya Mercedes Benz kugongana na trela. Picha|Boniface Mwangi

Dereva huyo ambaye alijeruhiwa vibaya, alikimbizwa katika Hospitali ya St Joseph kwa matibabu huku miili ya waathiriwa hao ikihifadhiwa katika mochari ya Hospitali ya Kaunti Ndogo ya Gilgil.

“Magari hayo yalivutwa hadi Kituo cha Polisi cha Gilgil kwa uchunguzi,” akasema Bw Ngaruiya.