Dondoo

Mfanyakazi apigwa na butwaa kugundua demu aliyeingia boksi ni ‘mali ya mkubwa’

Na JANET KAVUNGA October 9th, 2024 Kusoma ni dakika: 1

MTWAPA MJINI

POLO wa hapa alichanganyikiwa baada ya kugundua kuwa demu aliyemeza chambo aliyomrushia alikuwa mpango wa kando wa bosi wake.

Jamaa aliajiriwa katika hoteli moja ya hapa na akavutiwa na umbo na urembo wa kipusa mfanyakazi mwenzake.
Alijaribu bahati na demu akameza chambo mara moja.

Kwa kuwa mapenzi ni kikohozi hayafichiki, wafanyakazi wenzao walifahamu uhusiano wao na mmoja akaamua kumchanua jamaa.

“Huyu demu ni mali ya mdosi. Chunga usimwage unga ilhali ni vigumu kupata kazi siku hizi,” jamaa alimwambia jombi.

Hata hivyo, demu alikanusha madai hayo lakini akakiri bosi alimrushia mistari lakini hakuingia boksi.