• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 5:23 PM
Serikali yaomba wawekezaji kuisaidia kujenya nyumba za bei nafuu

Serikali yaomba wawekezaji kuisaidia kujenya nyumba za bei nafuu

Na BERNARDINE MUTANU

Serikali inalenga kuimarisha maeneo ya makazi ya gharama ya chini.

Kutokana na hilo, imetuma ombi kwa wawekezaji wa kibinafsi kuisaidia katika kuwekeza katika ujenzi wa nyumba za gharama ya chini nchini.

Katibu Mkuu wa Nyumba na Maendeleo ya Miji Charles Hinga alisema wote wanaolenga kushirikiana na serikali wana chini ya mwezi mmoja kutuma maombi.

Serikali ilifungua maombi hayo Jumatatu kwa Sehemu 1A, 1B na 1C.

Wote wanaolenga kuhusika watatuma maombi kwa kujaza fomu ya kimtandao, alisema Katibu huyo.

Kuambatana na mpango huo, serikali inalenga kujenga majumba 1,640 ya orofa Park Road, Starehe (3,500), Shauri Moyo (5,300), Social Housing (15,000) na Mavoko (5,500).

Kaunti zitakazoshirikishwa katika mpango huo zitanufaishwa na majumba

48,000 huku Nairobi na Mombasa zikitarajiwa kuwa na majumba mengi zaidi.

Mpango huo utazinduliwa katika muda wa miaka mitatu ijayo na tayari ekari 7,000 zimetengwa kwa ujenzi huo.

You can share this post!

KEPSA yakemea vikali mauaji ya 14 Riverside

Jacob Ojee ndiye nahodha mpya wa Shujaa

adminleo