Dondoo

Kidosho ahepa ‘date’ akihofia kutafunwa kabla avishwe pete

Na JANET KAVUNGA October 23rd, 2024 Kusoma ni dakika: 1

MAKUPA, MOMBASA

KIPUSA wa hapa aliwafichulia mashogake kuwa alikataa kwenda kwenye miadi Nairobi na mpenzi wake akihofia jamaa angemtafuna kabla ya kufunga ndoa rasmi.

Demu alisema mpenzi wake alipomwambia amepanga waende kutembea jiji kuu, alijifanya mgonjwa akishuku nia ya jamaa ilikuwa ni kumweka katika mtego amtafune ilhali alikata kauli ya kutomfungulia mzinga hadi watakapofunga harusi rasmi.

“Nilishuku mpango wake ni kutafuta fursa ambayo singeepuka kumwandalia asali kwa kuwa ingebidi tulale chumba kimoja. Nilicheza kama mimi kwa kujifanya mgonjwa hadi akaacha safari hiyo,” demu alisema.

Wenzake walimpongeza kwa ujanja wake wakisema mwanamume akionja tunda ni rahisi kutema mtu. Mwanamume huyo alikubali shingo upande na kuahidi kuandaa ziara nyingie siku tofauti.