Habari

Magenge yapora watu CBD Nairobi

Na WINNIE ONYANDO June 17th, 2025 Kusoma ni dakika: 1

MAGENGE ya watu waliobeba visu na marungu Jumanne Juni 17, 2025 walivuruga maandamano ya kudai haki kwa waathiriwa wa ukatili wa polisi na kupora wakazi katikati mwa jiji la Nairobi.

Watu hao walikuwa wamebeba marungu na visu wakitishia watu na kuwaibia.

Haikujulikana watu hao wanafadhiliwa na nani.

Haya yanajiri siku chache tu baada ya makundi ya sungusungu kupiga doria katikati mwa jiji la Nairobi yakiwa na mawe na nyahunyo wakati wa maandamano ya kudai haki kwa mwalimu-bloga Albert Ojwang aliyeaga dunia mikononi mwa polisi.

Hali hii ilifanya baadhi ya wafanyabiashara kufunga maduka yao kwa hofu ya kuporwa kama ilivyotokea wiki jana wakati wa maandamano ya kutaka haki kwa mwalimu-bloga Ojwang.

Maandamano ya Jumanne yalianza mwendo wa saa nne asubuhi.